KITISI FC watakutana na Kinyika FC kwenye mchezo wa fainali ya kombe la SPANEST katika tarehe itakayotangazwa baadaye baada ya kumalizika kwa maadhimisho ya wiki ya Utalii, ambayo kitaifa yanafanyika mjini Iringa kati ya Novemba 27 na 29, mwaka huu.
Wakati
Kitisi wamenusa fainali hiyo kwa mara ya pili baada ya kumchapa Mapagolo 5-1
katika mchezo uliopigwa Novemba 22, Kinyika imezima ndoto ya mabingwa wa mwaka
2014, Itundundu FC baada ya kuwachapa kwa mikwaju ya penati 4-3. Katika mchezo
uliochezwa Novemba 23.
Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Richard Kasesela alitoa zawadi ya Sh 20,000 kwa mchezaji wa Itunundu, Said Kisogenze aliyekuwa wa kwanza kuona lango la wapinzani wao, Kinyika.
Mbali
na mashindano hayo yaliyoshirikisha timu 24 zinazoundwa na vijiji
vinavyozunguka Hifadhi ya Taifa ya Ruaha, wilayani Iringa kuwasaidia wachezaji
wake kujenga afya, yanatumika kusambaza unaolenga kuwaokoa Tembo dhidi ya
majangili nchini kote.
Mratibu
wa Mradi wa Kuboresha Maeneo
Yaliyohifadhiwa Kusini mwa Tanzania (SPANEST) inayoratibu mashindano hayo, Godwell
Ole Meing’ataki alisema fainali ya ligi hiyo inalenga kuoa Tembo kwa kupitia
kauli mbiu yake ya “Piga Vita Ujangili, Piga Mpira Okoa Tembo.”
Meing’ataki alisema zawadi kwa
mshindi wa kwanza atakayepata kombe, medali, seti moja ya jezi, cheti na
kutembelea hifadhi ya Ruaha ataondoka na Sh Milioni moja taslimu, huku mshindi
wa pili atakayepata medali, cheti na mipira miwili atakinyakulia Sh 700,000.
Alisema timu ya Mapogolo FC na
Itunundu FC zitamenyana kusaka nafasi ya tatu ambayo mshindi wake atajipatia cheti
na medali na Sh 500,000 taslimu huku.
Meing’ataki alisema wazo la kuunganisha vijana
katika vita ya ujangili linaonekana kuwa njia muafaka ya kutokomeza ujangili
kutokana na ukweli kwamba vijana ndiyo walengwa wakubwa katika kushawishika
kuingia kwenye maeneo yaliyohifadhiwa na kufanya ujangili.
Alisema michezo hiyo itapigwa
katika uwanja wa Kimande, Pawaga kwasababu ya kuowa na mashabiki wenye mwamko
mkubwa wa mchezo huo.
0 comments:
Post a Comment