![]() |
MAMLAKA ya Udhibiti wa Huduma za Nishati
na Maji (EWURA) itaanza kutoa bei kikomo kwa gesi za kupikia zinazotokana na
zao la mafuta ya Petroli, utaratibu unaotarajia kuanza Januari mwakani.
Ikitangaza utaratibu huo, mamlaka hiyo
imesema muda wote, katika miundombinu ya kujazia gesi ya kupigia na vituo vya
kuuzia gesi ni lazima pawepo mizani inayoweza kupima uzito wa mitungi ya gesi.
Mkurugenzi wa Idara ya Petroli wa Ewura, Godwin
Samweli alisema mjini Iringa wakati mamlaka hiyo ilipofanya semeni na
wafanyabiashara wa mafuta wa mikoa ya Iringa na Njombe kwamba mizani hiyo ni
lazima iwe imehakikiwa na kuwekwa lakiri ya Wakala wa Vipimo Tanzania (WMA).
Alisema kutokuwa na mizani hiyo ni kosa
kisheria na adhabu kwa kosa la kwanza ni faini isiyopungua Sh Milioni 3, kosa
la pili faini isiyopungua Sh Milioni 5 na mkosefu mzoefu atanyang’anywa leseni.
Akifafanua kuhusu udhibiti wa bei ya gesi
ya kupikia, Samweli alisema baada ya EWURA kufanya mkutano na wadau wa sekta
hiyo baadaye mwaka huu, itakamilisha kanuni ya kupanga bei zitakazoanza
kutumika mapema mwakani.
Alisema mpango huo unakuja baada ya EWURA
kutengeneza utaratibu utakaoifanya Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (PBPA)
kuanza kuanza kuingiza gesi ya kupikia kwa wingi.
“Bei hizo zitakuwa zikitangazwa kama zile
za mafuta ya Petroli lakini kwasasa wafanyabiashara wazingatie bei zinazotolewa
na kampuni zinazowauzia gesi,” alisema.
0 comments:
Post a Comment