baada ya ajali hiyo, |
Inavyoonekana kwa nyuma |
hii ni sehemu ya mbele ya gari hilo |
Scania lililogongwa kwa nyuma |
Sehemu ambayo gari hilo dogo liliingia |
AJALI mbaya iliyohusisha gari dogo aina
ya Land Rover Freelander lenye namba T368 CVK na roli la mizigo aina ya Scania lenye namba T346 BRF imetokea usiku wa juzi katika eneo
la Lugemba, kilomita kadhaa kabla ya kufika mji wa Mafinga.
Taarifa za awali zinaonesha kwamba dereva
wa gari hilo jina lake bado halijapatikana alifariki papohapo baada ya gari yake
kuingia nyuma ya roli hilo lililokuwa limepaki kandakando ya barabara ya Mafinga Dar es Salaam, akiwa katika mwendo mkali.
Mwanafunzi wa kike wa Chuo Kikuu cha
Tumaini aliyekuwemo katika gari hilo amenusurika kufa; binti huyo ambaye pia
jina lake halikupatikana amelazwa katika hospitali ya wilaya ya Mufindi baada
ya kujeruhiwa vibaya ikiwa ni pamoja na kukatika mkono.
Mashuhuda wa tukio hilo wamesema ajali hiyo ilitokea majira ya saa 3 usiku. Na baada ya ajali hiyo wasamalia wema waliukumbiza mwili wa marehemu na majeruhi katika hospitali ya wilaya ya Mufindi.
Jeshi la Polisi limethibitisha kutokea
kwa ajali hiyo na taarifa za awali zinaonesha dereva wa gari hilo alikuwa
amelewa wakati akiendesha gari hilo.
Poleni sana madereva muwe makni
ReplyDelete